IJUE SAIKOLOJIA; ZIFAHAMU TABIA ZA MTOTO KULINGANA NA UMRI























Mazingira, malezi na familia ni mambo yanayochangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa mwili na akili ya mtoto, pamoja na uwezo wake wakutatua matatizo anayokumbana nayo katika maisha yake ya kila siku.


Uwezo wa kupambanua mambo baina ya mtoto na mtu mzima ni tofauti kabisa, Mfano; Mama anapovaa vizuri na kutaka kuondoka, mtoto huanza kulia akiamini kuwa mama anamuacha na hatorudi tena. Pia mtoto akiwa anachezea mpira na ukapotea ghafla, mtoto huusahau mpira ule kabisa na kuanza kuchezea vitu vingine. Katika hatua hii ya ukuaji, mtoto huamini kuwa vitu vinapoondoka mbele ya upeo wa macho yake havirudi tena na endapo vikirudi, basi mtoto hushituka sana.


Pia mtoto anapofikia umri wa kwenda shule, tunaweza kufikiri kuwa akili yake imekwisha kukua na anauweza wa kupambanua mambo kwa usahihi lakini, La Hashaah!!
             Mfano; Mtoto mwenye umri chini ya miaka saba, anaweza fikiri kuwa maziwa lita moja yakiwekwa kwenye vyombo vyenye maumbo na ujazo tofauti, basi maziwa hayo yanabadilika ujazo.

Hali hii huendelea hadi pale mtoto anapoweza kulinganisha au kuhusianisha taarifa alizonazo kwenye ubongo wake na zile ambazo anakutana nazo katika maisha ya kila siku.


Sasa tuangalie TABIA MBALIMBALI WANAZOONYESHA WATOTO BAADA YA KUZALIWA;


1.Miezi 0-1; Katika umri huu mtoto huweza kufanya tuu yale matendo yasiyo ya hiari ambayo hajafundishwa, mfano; Kunyonya maziwa ya mamye, kufumbua macho, kufumba macho. Pia katika umri huu, lugha kuu anayotumia mtoto ni lugha kama kulia wakati anasikia njaa, au kutabasamu au kucheka anapofurahi.


2.Miezi 1-4; Mtoto hupenda kurudia rudia kufanya vitu ambavyo anaona vinamfurahisha,
           Mfano; Mtoto anaweza kunyonya kidole kwa mara ya kwanza bila kukusudia, lakini baada ya muda anarudia kunyonya vidole kwa sababu aligundua anapata raha anaponyonya vidole vyake.

 3.Miezi 4-8; Mtoto huwa na tabia ya kurudia kurudia jambo kwa kusudi lakutaka kuona matokea yakufanya kitendo hicho yatakuwa nini?
            Mfano: Mtoto hujaribu kuinua kifani(toy) cha kuchezea na kujaribu kuweka mdomoni kusudi aone kama kinaweza kumpa raha kama anaponyonya ziwa la mama au kidole chake.


4. Miezi 8-12: Kwa kipindi hiki mtoto hufanya utafiti katika mazingira yanayomzunguka. Pia wakati huu mtoto huiga vitendo au tabia anazoona kwa watu wengine au watoto wenzake pindi anapocheza. Huweza kugundua vitu mbalimbali na tabia zake.
            Mfano; Mtoto anaweza kugundua kuwa akiangusha kijiko kinatoa mlio kinapofika kwenye sakafu, hivyo atajaribu kuangusha vitu vingine zaidi kama vikombe n.k ili kujua kuwa navyo vitatoa sauti au laah. (source-
www.africabongo.com)




0 comments: